Skip to main content

KUKOMESHA KISUKARI NI MIMI NA WEWE

KUKOMESHA KISUKARI NI MIMI NA WEWE


Ndugu msomaji nikukaribishe tena katika mwendelezo wa makala haya ya ugonjwa hatari wa kisukari kwa leo tukiangazia athari kubwa zinazowezasababishwa na kisukari karibu.
TULIPOISHIA MAKALA YALIYOPITA
Kwani kwa mujibu wa ripoti ya shirika la afya duniani(WHO)inadai magonjwa yasiyo ya kuambukiza ndio chanzo kikubwa cha vifo duniani yakifanya ongezeko ya vifo vyote kwa kila mwaka.
Inakisiwa kuwa mwaka wa 2020 magonjwa haya yasiyo ya kuambukiza yatasababisha asilimia 73 ya vifo vyote duniani na asilimia 60 ya ukubwa wa tatizo la magonjwa duniani.
SONGA MBELE ZAIDI..............
Kutokana na kuwepo kwa athari mbalimbali ambazo husababishwa na ugonjwa huu usiowa kuambukiza wa kisukari ni pamoja na kuwepo kwa uwezekano mkubwa kwa mgonjwa aliyekwisha kuathiriwa na kisukari wenda akapatwa na tatizo la figo .Japo ni vigumu kujua ni mgonjwa yupi wa ugonjwa wa kisukari anawezakukumbwa na tatizo hili la figo japo zipo ishara kadha wa kadha.
Ieleweke kuwa ugonjwa huu wa kisukari ni chanzo kikuu cha ugonjwa wa figo ulio katika hatua ya mwisho kutokana na walio wengi hupatwa na tatizo hili ,hata hivyo kwa mgonjwa wa kisukari ni vigumu sana kupatwa na tatizo la figo hasa katika kipindi cha miaka kumi ya kwanza kabisa ya tatizo la ugonjwa wa kisukari.
Ikumbukwe kuwa ugonjwa huu wa kisukari huorodheshwa na shirika la afya ulimwenguni kuwa ni moja ya sababu kuu za watu kufariki mapema ikiwa ni pamoja na kupatwa na matatizo ya upofu,figo kushindwa kufanya kazi inavyotakiwa ,mtu kukatwa mguu na kupatwa na ugonjwa wa kiharusi,kwani hali hii yote huchochea athari kubwa za kiuchumi hasa kwa mtu na hata familia kwa ujumla.
WHO katika kuangazia athari ya tatizo la ugonjwa huu hatari wa kisukari hasa kwa jamii za kimataifa katika kusaidia kinga uchunguzi na usimamizi unaotakiwa kwa ugonjwa huo ambao ulisababisha vifo vya takribani watu milioni 1.6 kwa mwaka 2016 pekee kote ulimwenguni.
Kuendelea kujitokeza kwa matatizo mbalimbali hasa haya yote huchochewa na kuwepo kwa tatizo hili la kisukari ambalo limekuwa tishio kubwa kwa maisha ya wanajamii mabalimbali,hata hivyo jitihada za haraka zinatakiwa kuendelea kuchukuliwa kutokana na hali halisi ya tatizo kuendelea kushika kasi kwa kuenea ulimwenguni kote.
Aidha, athari kubwa ya kiuchumi itokanayo na ugonjwa huu wa kisukari kuna uwezekano mkubwa kutokea kwa mtu yeye mwenyewe na familia kwa ujumla kwani gharama hiyo ya kupanda hali ya maisha yawezasababishwa na sindano ya Insulini na ufuatiliaji pekee ambao waweza kutumia nusu ya mapato kwenye familia hali inayowafanya walio wengi kushindwa kupata dawa za kisukari mara kwa mara na huduma husika hali inayochochea tatizo kubwa na kuendelea kuongeza idadi ya walioathiriwa na ugonjwa hatari wa kisukari.
Kutokana na tatizo hili kuendelea kushamiri na kuwa kubwa kwa kiasi chake hali inayoendelea kuleta athari kubwa kwa jamii ya kitaifa na kimataifa kwani ni wakati sasa kwa kila mmoja wetu kutambua ugonjwa huu kwa undani ikiwa ni pamoja na kufuatilia ushauri wa kitaalamu kuhusu afya yako ili kuanza kuchukua hatua za kukabiliana na ugonjwa huu ikiwa umebainika kuathiriwa.
Daktari mgeta anaeleza kwa ujumla jinsi ya kuepukana na tatizo hili kwa kuchukua tahadhari mapema ikiwa ni pamoja na jamii kuwa na utamaduni wa kujali afya kwa ujumla hapa anasema;
"Kwa ujumla jamii ijipe mtazamo wa kuwa inapima na kuchunguza afya baada ya muda fulani hasa baada ya mwezi unapashwa kuangalia afya yako kwa ujumla,pia mazoezi yapewe kipaumbele sana hali itakayoufanya mwili kuwa na kiwango cha sukari iliyo na uwiano sawa" alisema Mgeta.
Kutokana na hali halisi ya mambo yanayozidi kujitokeza kwa kasi sana kutokana na kuwepo kwa tatizo hili la ugonjwa wa kisukari ni hakika kwa pamoja kushirikiana kwa kiasi kikubwa na kwa nguvu moja katika kulitokomeza tatizo hili.licha ya tatizo hili kuendelea kuwa pana na lenye nguvu katika kukatiri uhai wa maisha ya watu walio wengi ulimwenguni wewe na mimi bado tunayo nafasi ya kutumia dawa katika kuondokana na hilo tatizo ikiwa ni pamoja na kuendele kuchunguza afya zetu kwa pamoja.
ENDELEA KUFUATILIA MWENDELEZO WA MAKALA MBALIMBALI ZA AFYA ZIJAZO...............
Suluhisho la tatizo ulilonalo kiafya ni hapa>>>>
Mawasiliano: +255782643285


Comments

Popular posts from this blog

Your Self Confidence

 Confidence  At the point when you're finding out about something new, it's not difficult to feel overpowered by the sheer measure of pertinent data accessible. This enlightening article should help you center around the essential issues.  So how would you stay quiet, formed and keep up confidence in an intense climate? Here are a few hints you may to consider as a starter manual for personal development.  Envision yourself as a Dart Board. Everything and every other person around you may become Dart Pins, at some point. These dart pins will wreck your confidence and pull you down in manners you wont even recall. Dont let them demolish you, or bamboozle you. So which dart pins would it be advisable for you to stay away from?  Dart Pin #1 : Negative Work Environment  Be careful with brutal hypothesis where every other person is battling just to excel. This is the place where non-grateful individuals normally flourish. Nobody will value your commitments regar...

A Million Dollar Smile for Healthy Teeth

  Glaring Tips On Teeth Whitening, Making That Smile Look Better Staring your day with a frown face will not give you any luck. The best way to have a beautiful day is to have a beautiful smile. Having a beautiful smile is having clean and white bright teeth. The first thing that you notice to a person when having a conversation is their teeth. Healthy bright white teeth always get special and extra attention. Nowadays, people are more conscious on how their teeth look like. As much as possible, a person wants to have strong and healthy white teeth. In order for the people to have white teeth they would tend to use teeth whitening. However, not all teeth whitening are advisable for the consumers. There can be a lot of side effects that may occur in making use of teeth whitening. Using teeth whitening can cause problem in your teeth, gums or even to your health in general. Fortunately, there is a product to  keep your teeth strong and healthy from childhood to old age. Here’s h...

Real Estate Investment – One Simple Formula

 I saw the advertisements in our humble community paper for quite a long time before I understood precisely what was happening. They were consistently the equivalent: A house available to be purchased with 5% down and installments of 1% of the price tag. It very well may be a three room home for $90,000, for instance, with $4,500 down and $900 every month installments.  A companion began doing likewise and disclosed the cycle to me. It was an approach to get an incredible profit for capital. It was something contrary to purchasing with no cash down. You purchased for money.  A Real Estate Investment Formula  It is basic, truly. At the point when you purchase for money, you frequently improve cost. A house that needs a little work may be valued at $75,000, for instance. By offering $65,000 money, you arrange your way to a $68,000 price tag. If not, you leave – there are consistently others.  At that point you put not many thousand into exceptional yield fixes and...